Wanawake Wakulima wa Afrika Wanapambana na Athari ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa
Na Ronald Joshua
NEW YORK | BAMAKO (IDN) – Fatou Dembele ni mkulima katika nchi ya Mali isiyo na bandari, ambapo nusu ya wakazi wanaohusika katika kilimo ni wanawake. Kilimo ni sekta muhimu ya kuinua wanawake kutokana na umasikini. Lakini uharibifu unaoongezeka wa ardhi na rasilimali za asili unaosababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa unawafanya wanawake wawe katika hatari zaidi.
Kwa hivyo wakati mimea ya Dembele ilianza kufa, alifikiri shamba hilo liliharibiwa, na maisha yake yalikuwa katika hatari. “Tulifikiri shamba lilikuwa na ugonjwa. Hatukujua ya kwamba kulikuwa na vimelea vya kuishi vilivyoshambulia mizizi ya mimea na kuweza kuiua,” anasema Dembele.…