Home – SDGs for All

A project of the Non-profit International Press Syndicate Group with IDN as the Flagship Agency in partnership with Soka Gakkai International in consultative status with ECOSOC

Watch out for our new project website https://sdgs-for-all.net

Photo: Members of the women's cooperative use climate-resilient organic compost and biopesticides in their farm. Credit: UN Women

Wanawake Wakulima wa Afrika Wanapambana na Athari ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa

share
tweet
pin it
share
share

Na Ronald Joshua

NEW YORK | BAMAKO (IDN) – Fatou Dembele ni mkulima katika nchi ya Mali isiyo na bandari, ambapo nusu ya wakazi wanaohusika katika kilimo ni wanawake. Kilimo ni sekta muhimu ya kuinua wanawake kutokana na umasikini. Lakini uharibifu unaoongezeka wa ardhi na rasilimali za asili unaosababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa unawafanya wanawake wawe katika hatari zaidi.

Kwa hivyo wakati mimea ya Dembele ilianza kufa, alifikiri shamba hilo liliharibiwa, na maisha yake yalikuwa katika hatari. “Tulifikiri shamba lilikuwa na ugonjwa. Hatukujua ya kwamba kulikuwa na vimelea vya kuishi vilivyoshambulia mizizi ya mimea na kuweza kuiua,” anasema Dembele.

Idadi iliyoongezeka ya vimelea, kwa sababu ya kupanda kwa joto na unyevu, ni moja tu ya madhara mengi ya mabadiliko ya hali ya hewa ambayo Dembele na wanawake wakulima wengine wanakabiliwa nayo.

Ili kupambana na athari mbaya ya mabadiliko ya hali ya hewa juu ya maisha ya wanawake, mpango mpya wa Wanawake wa Umoja wa Mataifa unaojulikana kama Agriculture Femmes et Développement Durable (AgriFed), uliotekelezwa na shirika la ndani/mitaa lisilo la kiserikali la Groupe d’Animation Action au Sahel (GAAS) Mali, unasaidia wazalishaji wa mitaa kufanya marekebisho kukabiliana na changamoto hizi mpya.

Mpango huo hufanya kazi na wakulima ili kufanya mbinu zao kuwa za kisasa, huwezesha upatikanaji wao wa habari juu ya maendeleo ya hivi karibuni katika kilimo na huongeza thamani ya mazao yao kwa kuboresha njia zao za uhifadhi.

“Athari za mabadiliko ya hali ya hewa haziwachi nchi ya Mali, na zinadhuru nchi hii zaidi, changamoto zaidi katika muktadha wa usalama hafifu sana katika eneo la Sahel,” Maxime Houinato, Mwakilishi wa Nchi wa Wanawake wa Umoja wa Mataifa nchini Mali, alisema katika tukio la upande lililoandaliwa na Wanawake wa Umoja wa Mataifa tarehe 14 Machi katika mkutano wa 62 wa Tume ya Umoja wa Mataifa juu ya Hali ya Wanawake (CSW62). 

“Hata hivyo, nchi ya Mali, ingawa ni mchangiaji mdogo wa utoaji wa gesi ya asili, ina nia ya kupambana ili kurekebisha njia ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya hali ya hewa,” aliongeza.

Ili kurejesha uzalishaji wa Dembele, mpango huo ulimfundisha jinsi ya kutumia vifaa vya asili vya kuua vimelea vilivyopo ndani ya nchi ili kuondoa vimelea. “Shukrani, tulijifunza ya kwamba kuna mimea ya ndani ambayo miche yake inaweza kupambana na ugonjwa huu,” anasema Dembele.

AgriFed ilianza shughuli zake mwaka wa 2017 katika eneo la Segou, zaidi ya kilomita 200 kaskazini mashariki mwa Bamako, mji mkuu wa Mali. Mafunzo juu ya mbinu endelevu za kilimo yalifikia wanawake 247 na wanaume 66. Mafunzo yalisaidia wakulima kuboresha matumizi ya maji, ratiba ya mazao, matumizi ya dawa ya kuua vimelea na mbolea, na mbinu za kulima.

Katika miji ya Boidié na Sécoro, na Cercle de Tominan, wanawake wameboreshwa na kuongeza uzalishaji wa mimea aina ya vitunguu, shukrani kwa mafunzo. Lakini wakati wa mavuno, ikawa wazi ya kwamba wanawake walihitaji kujifunza jinsi ya kuhifadhi mazao yao bora.

“Tunapanda mimea aina ya vitunguu na vitunguu kwa sababu ya maisha yake ya muda mrefu, lakini hatukujua mbinu za kuhifadhi [kabla],” alieleza Hayèrè Keita, mzalishaji wa mmea aina ya kitunguu na muuzaji huko Sécoro. “Kufuata mbinu zetu za jadi, viwango vya kupoteza vinaweza kuwa juu sana.”

Wanawake wa Umoja wa Mataifa waliunga mkono vikao vya mafunzo zaidi ambavyo vilionyesha wakulima jinsi ya kuhifadhi mazao ya mimea aina ya vitunguu, vitunguu na viazi. Karibu wazalishaji wanawake 110 wameweza kuongeza mapato yao kwa kutumia mbinu hizi za kisasa za uzalishaji na uhifadhi.

“Nimekuwa nikipanda mboga na matunda kwa miaka 20, lakini nilijua tu njia ya jadi ya kufanya hivyo,” anasema Alphonsine Dembele, mkulima mwingine.

“AgriFeD ilitufundisha kupanua mazao ambayo tunapanda, na kuanzishwa kwa viazi, nyanya na pilipili. Hayaleti tu mapato ya ziada, lakini pia husaidia kuboresha lishe nyumbani na kupunguza ukosefu wa lishe bora kwa watoto wetu. anasema Dembele, mkulima mwingine.

Anaongeza: “Imekuwa na ushawishi mzuri juu ya ushirikiano wa kijamii, kwa sababu wanawake [kutoka kwa jamii mbalimbali za kikabila] sasa wanakutana na kuwa na mazungumzo wakati wa mikutano ya mafunzo mashambani.”

Mpango huo, uliofadhiliwa na Serikali ya Luxembourg, utaendelea kwa miaka mitano na unatarajiwa kuingizwa katika maeneo mengine ya nchi.

Mpango ulizinduliwa Desemba 12, 2017 na lengo la kujenga ujasiri wa wanawake na vijana milioni huko Sahel kwa athari za hali ya hewa kupitia kilimo mahiri katika One Planet Summit. Uzinduzi huo ulihusishwa na mkusanyiko wa viongozi wa dunia katika mji mkuu wa Kifaransa kuadhimisha kumbukumbu ya Mkataba wa Mabadiliko ya Hali ya Hewa wa Paris.

Mkutano wa One Planet Summit, uliosimamiwa na Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres, na Rais wa Benki ya Dunia, Jim Yong Kim, ulikuwa na lengo la kusaidia mchakato rasmi wa Umoja wa Mataifa kuhusu hatua ya hali ya hewa huku mataifa yakitazamia kuinua tamaa ya hali ya hewa katika mchakato hadi 2020.

Mpango huo ni mpango wa Mkakati Jumuishi wa Umoja wa Mataifa wa Sahel (UNISS) na Sekretarieti ya G5. G5 Sahel, mfumo wa taasisi ya uhamasisho wa maendeleo miongoni mwa nchi tano katika kanda – Burkina Faso, Chad, Mali, Mauritania, na Niger – umetambua kupambana na mabadiliko ya hali ya hewa na uharibifu wa mazingira, pamoja na athari zake juu ya wakazi wa vijijini, kama kipaumbele.

Katika ngazi ya kitaifa, serikali zinafanya kazi juu ya mikakati ya kukabiliana na hali; mpango mpya umebuniwa kusaidia juhudi hizo. Wanawake wa Umoja wa Mataifa waliwasilisha mpango, ambao ni baadhi ya 12 zilizoonyeshwa kwenye Mkutano, kwa niaba ya mfumo wa Umoja wa Mataifa. [IDN-InDepthNews – 27 Machi 2018]

NEWSLETTER

STRIVING

MAPTING

PARTNERS

Scroll to Top