Home – SDGs for All

A project of the Non-profit International Press Syndicate Group with IDN as the Flagship Agency in partnership with Soka Gakkai International in consultative status with ECOSOC

Watch out for our new project website https://sdgs-for-all.net

Waafrika Wanaapa Kukuza ujenzi wa Viwanda wenye Ushirikiano na Uendelevu

share
tweet
pin it
share
share

Uchambuzi na Jeffrey Moyo

HARARE (IDN) – Jukwaa la tatu la Maendeleo lenye Uwezo wa Kiafrika lililoandaliwa na Msingi wa Ujenzi wa Uwezo wa Kiafrika (MUUK), kwa ushirikiano na wadau wa shirika la Kiafrika na washirika wa kimataifa, wameapa kuboresha sekta ya viwanda pamoja na miundombinu, ili kukuza ujenzi wa viwanda wenye ushirikiano na uendelevu na kuendeleza ubunifu katika njia moja na lengo la tisa la Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Kimataifa.

Kama vile, shirika hilo linasema limewekeza zaidi ya dola bilioni moja, kujenga taasisi katika nchi arobaini na tano katika bara la Afrika na kusaidia jumuiya za kikanda za kiuchumi pamoja na mashirika ya bara.

SDG zilijengwa kwenye malengo manane ya kupambana na umaskini ambapo dunia ina nia ya kufanikisha ifikapo mwaka wa elfu mbili na kumi na tano, jina la Malengo ya Maendeleo ya Milenia.

Kongamano la ACBF, kutoka Mei tarehe mbili hadi tarehe tano mjini Harare, mji mkuu wa Zimbabwe, ulilenga kuwezesha bara lenye maendeleo duni kwa kulenga katika ujenzi wa miundombinu barani Afrika.

Kongamano la ACBF la mwaka huu lilikuwa na mbio chini ya kaulimbinu Kukuza Uwezo kwa Uchumi na Mabadiliko ya Kijamii ya Afrika’. Kongamano pia lilikuja wakati shirika lilikuwa linasherehekea Jubilei yake ya Fedha, hii ni baada ya kuanzishwa katika mwaka wa elfu moja tisini na moja na serikali za Afrika na washirika wao wa kimaendeleo ili kusaidia kujenga uwezo endelevu wa binadamu na taasisi kwa ajili ya utawala bora na usimamizi wa maendeleo.

Kwa hili, shirika lilitoa wito kwa serikali za Afrika kufanya kazi kuelekea kuendeleza miundombinu barani Afrika.

“Mawaziri wa Fedha na Mipango, mashirika ya kimataifa, wafadhili, wasomi na wawakilishi kutoka taasisi zinazoungwa mkono na ACBF wanapaswa kuzingatia vipimo vya uwezo kwenye Agenda ya Umoja wa Afrika 2063 na Malengo Endelevu ya Maendeleo,” katibu mtendaji wa ACBF Emmanuel Nnadozie, alisema katika kongamano hilo.

Hii, alisema, itafanyika kwa msisitizo juu ya jukumu la serikali, washirika wa maendeleo, asasi za kiraia, sekta binafsi, taasisi za mafunzo na vyombo vya habari katika kusaidia uwezo wa maendeleo kwa ajili ya mageuzi ya kiuchumi na kijamii barani Afrika.

Nnadozie anaamini kwamba hakuna linalopaswa kutowezekana kwa Afrika wakati inakubaliwa kuleta maendeleo endelevu yenyewe. Baadhi ya uchumi unaokua kwa kasi duniani, alisema, umesonga hatua mbele katika kufikia SDG za Umoja wa Kimataifa kwamba wao wamepata mafanikio yao kupitia mkakati wa uwekezaji katika uwezo wa binadamu, taasisi na mashirika.

Sambamba na SDG kupitishwa na viongozi wa dunia katika Septemba mwaka wa elfu mbili na kumi na tano kuongeza upatikanaji wa makampuni madogo madogo ya viwanda na mengine, ACBF pia walifanya wito kwa kuongezeka kwa viwanda katika bara zima.

“Ukuaji halisi wa kasi, umoja, mageuzi na usawa si chaguo tena, lakini muhimu kwa ajili ya Afrika ili, katika njia muhimu, kujenga kazi, kukabiliana na umaskini na kupata umoja na maendeleo endelevu ya kijamii na kiuchumi haraka,” Kamishna wa Mambo ya Kiuchumi wa Umoja wa Afrika Anthony Mothae Maruping, aliambia IDN.

Na lengo la tisa la SDG pia linatoa wito kukuza umoja na ujenzi endelevu wa viwanda na, ifikapo mwaka wa elfu mbili na thelathini, kwa kiasi kikubwa kuongeza kushiriki sekta ya ajira, Maruping alisema: “Mseto wa kuongeza thamani utasababisha ukuaji wa kazi na uchumi kwa kasi na umoja ambao unastahimili zaidi kwa majanga ya nje na, hata kweli ya ndani.”

Lakini Afrika haina ujuzi wa kutosha kuokoa yenyewe ukuaji wake wa viwanda, kwa mujibu wa ACBF. Kama vile, kwa mujibu wa Maruping, ACBF pia wanapaswa kuzingatia ujuzi wa binadamu kama sehemu ya jitihada za kupunguza mtaji wa watu kukimbia ndani ya bara la Afrika. Yeye anaonekana kuwa katika mkataba na Profesa Emmanuel Nnadozie, Katibu Mtendaji wa ACBF.

“Ili kufanikisha mabadiliko ya kiuchumi, kisiasa na kijamii, tutahitaji ujuzi muhimu na mabadiliko ya mawazo” Profesa Nnadozie alisema. Alipoulizwa kufafanua juu ya ni nini maana ya hiyo katika hali halisi, Nnadozie alisisitiza haja ya kuendeleza ujuzi, kama vile wahandisi zaidi, wataalamu wa kilimo zaidi, na mameneja zaidi.

Nnadozie alisema kuwa kwa sasa Afrika ilikuwa na pengo la wahandisi milioni nne nukta tatu kama bara lilikuwa litekeleze miradi yake yote. “Tunahitaji wanasayansi wa kilimo na watafiti milioni moja nukta sita; tumebainisha pengo la wahandisi wa maji na usafi milioni mbili nukta nane. Na hii inahusiana na mahitaji yaliyolengwa yaliyotambuliwa kwa ajili ya mwaka wa elfu mbili ishirini na tatu – miaka kumi iliyolengwa kwa hatua ya kwanza ya Afrika mwaka wa elfu mbili sitini na tatu”.

Hivi sasa zaidi ya asilimia themanini ya wanafunzi wanajiandikisha katika sayansi ya jamii na masomo ya kibinadamu na kuna haja ya juhudi za makusudi shina mwenendo huu na kuelekeza wanafunzi zaidi kuelekea taaluma shina (sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati).

Nchi katika bara zitahitajika kuboresha uwezo wake wa mashirika na watu kuwa na uwezo wa kufikia malengo yaliyowekwa chini ya Agenda ya Umoja wa Afrika mwaka wa elfu mbili ishirini na tatu kama vile UNSDG.

Hata hivyo, ukosefu wa fedha umeonekana kuwa changamoto kubwa kwa bara linaloendelea, na ACBF kuwa endelevu na fedha za wafadhili, na hii wakati wito unakuwa na sauti zaidi kwa serikali za Afrika kusimamia shirika lao wenyewe.

Lakini hii inaweza kuwa kazi kubwa kwa nchi nyingi kama Zimbabwe ambayo uchumi wake unaningínia na kamba nyembamba.

Waziri huyu wa Fedha na Maendeleo ya Uchumi wa nchi ya Afrika ya Kusini, Patrick Chinamasa amekuwa kwenye rekodi katika vyombo vya habari akisema kurekebisha uchumi wa nchi zenye wasiwasi kunahitaji ushirika wa wadau.

Lakini kama kwa UNSDG kusaidia maendeleo ya kiuchumi na ustawi wa binadamu, kwa lengo la upatikanaji nafuu na usawa kwa wote, inabakia kuonekana kama ACBF watasimamia kutoa baadhi ya majibu kwa ongezeko la ole ya kiuchumi ya bara. [IDN-InDepthNews – Tarehe nane, mwezi Mei, mwaka wa elfu mbili kumi na sita (8/5/2016)]

IDN ni wakala wa Chama cha Vyombo vya habari vya Kimataifa.

NEWSLETTER

STRIVING

MAPTING

PARTNERS

Scroll to Top