Home – SDGs for All

A project of the Non-profit International Press Syndicate Group with IDN as the Flagship Agency in partnership with Soka Gakkai International in consultative status with ECOSOC

Watch out for our new project website https://sdgs-for-all.net

ICPD25 Inaonyesha Njia ya Kupata Haki za Wanawake na Wasichana

share
tweet
pin it
share
share

Na Justus Wanzala

NAIROBI (IDN) – ICPD25, mkutano uliofanyika Nairobi jiji kuu la Kenya kuanzia Novemba tarehe 12-14 na kuashiria maadhimisho ya miaka 25 ya Mkutano wa Kimataifa wa mwaka wa 1994 juu ya Idadi ya watu na Maendeleo (ICPD) mjini Cairo, Misri, uliishia na ahadi ya ujasiri kufikia kupatikana kwa haki za wanawake na wasichana.

Mkutano, uliohudhuriwa na viongozi wa ulimwengu zaidi ya 6,000, wasomi, watetezi wa haki na viongozi wa imani waliona washirika wakitangaza kujitolea kumaliza vifo vyote vya akina mama, kutosheleza hitaji ambalo halikutimizwa la upangaji wa uzazi na kukabiliana na unyanyasaji wa kijinsia na shughuli hatari dhidi ya wanawake na wasichana ifikapo mwaka wa 2030.

Mkutano ulioitishwa na serikali za Denmaki na Kenya pamoja na Hazina ya Idadi ya watu ya Umoja wa Mataifa (UNFPA), mkutano ulilenga kutoa jukwaa la pamoja, kuleta pamoja serikali, mashirika ya Umoja wa Mataifa, asasi za kiraia, mashirika ya sekta za kibinafsi, makundi ya wanawake na mitandao ya vijana.

Washiriki waligundua kuwa kupatikana kwa Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDGs) hakuwezi kufikiwa isipokuwa wanawake, wasichana na vijana wanadhibiti miili yao, maisha yao, na wanaishi bila vurugu.

Mkurugenzi Mtendaji wa UNFPA Natalia Kanem alisema Mkutano wa Nairobi uliwakilisha maono yaliyofanywa upya na yaliyotiwa nguvu upya na jumuiya ya kufanya kazi pamoja kutenda na kutoa matokeo. Aligundua kuwa kupitia umoja, miaka kumi ijayo inaweza kuwa muongo wa hatua na matokeo kwa wanawake na wasichana.

Mkutano huo pia ulifunua data mpya kuhusu gharama ya kufikia malengo yaliyowekwa. Kwa mujibu wa uchambuzi na UNFPA na Chuo Kikuu cha Johns Hopkins, kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Victoria, Chuo Kikuu cha Washington na shirika la Afya la Avenir, jumla ya gharama kwa dunia kufikia malengo ingekuwa dola bilioni 264.

Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari, Kanem alieleza kwamba uwekezaji huu unatumika kufikia malengo matatu: 1) hitaji ambalo halijatimizwa la kuzuia mimba, kwa kila mwanamke na vijana wasichana kufanya maamuzi juu ya kama au wakati gani wa kuwa na mimba, na kiasi cha watoto wa kuwa nao; 2) vifo vya wamama vinavyoweza kuzuiwa, ili kwamba hakuna mwanamke anayepoteza maisha kwa kukosa huduma ya afya ya uzazi; na 3) bila unyanyasaji wa kijinsia na bila kesi za ukeketaji, pamoja na ndoa za watoto na za lazima.

Kanem alisema, “Sitaki kutaja dola bilioni 264 kama gharama lakini ni kama uwekezaji katika ubinadamu. Ni gharama ambayo hatuwezi kuzuia kubeba.” Hesabu hii itajumuisha dola milioni 7.5 katika uwekezaji mpya kwa miaka pamoja na uwekezaji wa kiufundi kwa kuchochea uvumbuzi na ustadi wa sekta binafsi kufikia upatikanaji wa ahadi ya Nairobi.

Kiongozi wa UNFPA alisisitiza kwamba ICPD inajumuishwa, bila kundi lililotengwa ikiwa ni pamoja na wasagaji, mashoga, jinsia mbili na wasenge jamii ya (LGBT) kuwachwa nje.

Mkutano ulitoa fursa kwa makundi yaliyotengwa kama vile vijana na mawakili wa mashinani kujihusisha na wakuu wa nchi na watunga sera kuhusu jinsi ya kutambua haki na afya ya watu wote.

Kufuatilia upya nyayo na wakati huo huo mtazamo wa makini ndani ya baadaye, Kanem aliwaambia wajumbe kuwa licha ya safari ndefu mbele, maendeleo yamepatikana katika miaka 25 iliyopita tangu mkutano wa Cairo. “Vifo vya akina mama vimeshuka kwa asilimia 44 ulimwenguni kote,” alisema Kanem, na kuongeza: “Hii inamaanisha wanawake milioni nne ambao wangekuwa pengine wamekufa wakiwa wajawazito, au wakati wa kujifungua, wako hai leo” lakini “maendeleo mazuri hayatoshi, na ahadi zilizotolewa kwa wasichana, wanawake na kila mtu zinapaswa kutimizwa.”

Kwa njia ya ahadi, serikali za nchi mbalimbali – kati yao Austria, Kanada, Denmaki, Ufini, Ufaransa, Ujerumani, Iceland, Italia, Uholanzi, Norwe, Uswidi na Uingereza, pamoja na Tume ya Ulaya – ziliahidi dola bilioni moja. Sekta ya kibinafsi iliwakilishwa na mashirika kama vile Ford Foundation, Johnson & Johnson, Philips, World Vision na mashirika mengine mengi yaliahidi kuchanga karibu dola bilioni nane.

Akihutubia mkutano, Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta alisema ulimwengu umebadilika sana tangu mwaka wa 1994 katika uwanja wa idadi ya watu na maendeleo. “Kukosekana kwa usawa kumeongezeka ndani na kote nchini na kuna utofauti mkubwa sana wa idadi ya watu. Nchi zingine ulimwenguni zinakabiliwa na uzee wa haraka wa watu; wakati zingine zinajitayarisha kwa kikundi kikubwa zaidi cha vijana ambao ulimwengu umewahi kuona,” alisema.

Akitoa wito wa kuondoa vitendo, sera na sheria ambazo zinadhoofisha haki za wanawake, Kenyatta alisema kuna haja ya kuondoa ukeketaji (FGM) ambao, alisema, unabakia moja ya ukiukwaji mkubwa zaidi wa haki za binadamu za wanawake na wasichana. “Mnamo Aprili mwaka huu tulitia saini tamko muhimu kati ya serikali za Kenya, Uganda, Tanzania, Somalia na Uhabeshi ili kuzungumzia kitendo cha ukeketaji (FGM) mpakani,” alisema.

Alitoa wito kwa washiriki kuzingatia wale aliowaita “washiriki muhimu zaidi” waliokosekana mkutanoni, akidokeza kwa waathirika wa uhasama wa kijinsia, ubaguzi na unyanyasaji. “Ninamaanisha wanawake 1-katika-5 kutoka kila pembe ya dunia ambao mwaka huu peke yake watapitia uhasama wa kijinsia, uwezekano mkubwa kutoka kwa mtu wa karibu nao; wanawake na wasichana 800 wanaokufa kila siku wakati wa ujauzito au kujifungua; na wasichana milioni nne ambao, kila mwaka, wanapaswa kuvumilia uchungu na madhara ya kiwewe cha ukeketaji (FMG),” alisema.

Uhuru aliongeza kuwa kategoria zingine ambazo hazishiriki lakini muhimu ni wasichana zaidi ya 33,000 ambao wanaingizwa katika ndoa kila siku kabla ya umri wa miaka 18, na mamilioni ya vijana wasio na ajira ambao hawana tumaini kamili la maisha yao ya baadaye.

Ib Petersen, Mjumbe Maalum wa Denmaki wa ICPD25, alisema hakutakuwa na ICPD50, na kuongeza kuwa wanawake na wasichana ulimwenguni kote wamesubiri muda mrefu wa kutosha kuwa na haki na uchaguzi. “Tunapoelekea 2030, sasa tunaingia muongo wa uwasilishaji ambao tutazungumza na kujitolea sote kwa ahadi tulizopeana jijini Nairobi,” alisema Petersen.

Rasmus Prehn, Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Denmaki, aliitisha msaada zaidi kwa vijana na wanawake, akibainisha kuwa wanawake na wasichana waliosemwa wako kwenye moyo wa maendeleo endelevu. “Wanawake na wasichana ndio wamiliki wa kweli wa miili yao,” alisema.

Maoni yake yalirejelewa na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina Mohammed, aliyesema: “Mamilioni ya wanawake na wasichana bado wanangojea ahadi kutimizwa, wamekuwa wakingojea kwa muda mrefu. “Aliongeza kwamba SDGs haziwezi kupatikana mpaka wanawake, wasichana na vijana wawe na uwezo wa kudhibiti miili yao na maisha yao, na kuishi bila uhasama.”

Balozi Kamau Macharia, Katibu Mkuu katika Wizara ya Mambo ya Kigeni ya Kenya, aliwaambia wajumbe kuwa “kama nchi inayoendelea tunajua gharama ya kukosa maendeleo: gharama ya akina mama waliokufa, yatima, waliotolewa mimba na familia zilizovunjwa na uhasama wa kijinsia vinaaibisha hizo dola bilioni 264.”

Kulingana na Macharia, mataifa yanayoendelea hayapaswi kungojea wafadhili ili wafadhili mipango yao bali zinapaswa kuhamasisha ufadhili wao wenyewe. “Nchi zinazofanya jitihada ni zile zinazotumia rasilimali zao kufadhili miradi yao zenyewe ndani ya ajenda ya kimataifa.” [IDN- InDepthNews – 17 Novemba 2019]

Picha: Nairobi I CP D25 Mkutano wa Nairobi unafungwa na wito wa kuchukua hatua. Hisani: Flckr | UNFPA

NEWSLETTER

STRIVING

MAPTING

PARTNERS

Scroll to Top