Home – SDGs for All

A project of the Non-profit International Press Syndicate Group with IDN as the Flagship Agency in partnership with Soka Gakkai International in consultative status with ECOSOC

Watch out for our new project website https://sdgs-for-all.net

Athari ya COVID-19 Inakumba Afrika – Video Iliyohuishwa Inawaambia Watoto Kuihusu

share
tweet
pin it
share
share

Na Lisa Vives, Mtandao wa Taarifa wa Kimataifa

NEW YORK (IDN) – Wakati Afrika, kama jamii ya kimataifa kwa ujumla, inashiriki katika vita vikali dhidi ya virusi vya korona, mtaalamu wa Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) ameuliza kuhusu makadirio ya kutisha ya wale walioathiriwa na COVID-19. Wakati huo huo, Ghana kwa hatua ya mshangao imeamuru kuondolewa kwa kusitishwa kwa shughuli za kawaida kwa kiasi fulani. Kirusi kilichoenea sana kinaingiza Rwanda katika ‘mikopo’ mikubwa chini ya upunguzaji wa deni.

Video iliyohuishwa

Mtengeneza sinema maarufu wa Nigeria Niyi Akinmolayan ameunda video iliyohuishwa ili kuwasaidia vijana kuelewa kwanini wanapaswa kukaa nyumbani na kuhairisha michezo ya nje na marafiki wao. Hapo ndipo jinamizi la katuni ya Akinmolayan inaingia.

Katika uhuishaji wa sekunde 90, uhuishaji unaelezea hadithi ya ndugu wawili, Habeeb na Funke. Habeeb anachoka kukaa nyumbani na kuamua kutoka nje kisiri kucheza soka. Dada yake mkubwa Funke, akiosha mikono yake, anamwonya asiende nje, lakini anasisitiza, na kukabiliwa tu na jinamizi la kijani lenye sura mbaya!

Akinmolayan, anayejulikana sana kwa kuongoza “Harusi Sehemu ya 2 (The Wedding Party 2)”, filamu iliyoenea zaidi ya Nigeria, alisema alihamasishwa baada ya majaribio kadhaa kuelezea kusitishwa kwa shughuli za kawaida kwa mwanawe mwenye umri wa miaka 5.

“Lakini bado hakuelewa mpaka nikabadilisha hadithi na kusema virusi vya korona kweli vinafanana na jinamizi kubwa na viko huko nje barabarani na ukienda vitakukamata,” aliiambia Reuters.

Ezichi Nwaogu, 9, alielezea sehemu yake aliyoipenda zaidi ni wakati mvulana huyo alifungua mlango na kuona virusi vya korona, jinamizi, nje, kisha akasukuma mlango kwa nguvu na ikambidi aingie ndani. “Sasa najua kuwa huu sio wakati sahihi wa kwenda mahali popote au nje,” alisema.

Akinmolayan alifanya uhuishaji kupitia kampuni yake ya utengenezaji, Anthill Studios, akitumia kikosi imara cha watu 10 wote wanaofanya kazi kando kando kutoka manyumba mwao.

Inasambazwa bure na inaweza kupakuliwa kwa Kiingereza, Kiigbo, Kiyoruba, Kihausa, Kifaransa na Kiswahili. https://we.tl/t-EBxBabZaxt

Makadirio ya kupita kiasi

Kulingana na kielezo cha muda, mahali popote kati ya maelfu na mamilioni ya Waafrika huenda wakaambukizwa na virusi vya korona. Lakini hesabu hii ya kutisha ya msemaji wa eneo wa WHO ilibishwa na mkuu wa shughuli za dharura kwa WHO Afrika.

“Hii bado inapaswa kutengenezwa vizuri,” Michel Yao alisema kwenye kongamano la njia ya simu la vyombo vya habari. “Ni vigumu kufanya makadirio ya muda mrefu kwa sababu muktadha unabadilika sana.” Pia, aliongeza, “hatua za afya ya umma zinapotekelezwa kikamilifu zinaweza kweli kuwa na matokeo.”

Yao alibainisha kuwa utabiri kama huo wa kisa kibaya zaidi kwa mkurupuko wa Ebola haukutimia kwa sababu watu walibadilisha tabia mapema.

Kufikia sasa, kumekuwa na visa 17,000 vilivyothibitishwa vya ugonjwa wa COVID-19 kwenye bara la Afrika na karibu vifo 900 – kiasi kidogo ukilinganisha na maeneo mengine.

Maambukizi nchini Afrika Kusini, ambayo ina idadi kubwa ya visa, yamepungua baada ya kuzindua kusitishwa madhubuti kwa shughuli za kawaida, lakini mataifa mengine – kama Burkina Faso, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Algeria – yameona juu kuliko hali mbaya ya wastani.

WHO inafanya kazi na mamlaka huko kuboresha huduma ya mgonjwa na kupunguza vifo/hali mbaya, alisema Matshidiso Moeti, mkurugenzi wa WHO eneo la Afrika, yanayojumuisha mataifa 46 ya Sahara-ndogo na Algeria.

Juhudi hizi, hata hivyo, zinawezakuwa zimesitishwa na mashambulizi ya hivi karibuni ya Rais Donald Trump kwenye shirika la afya la Umoja wa Mataifa ikiwa ni pamoja na tishio lake la kuondoka ufadhili wa kifedha kwa shirika.

Hii inaweza kuathiri mapambano dhidi ya virusi na dhidi ya magonjwa mengine yanayoweza kulemaza na yanayotishia maisha kama polio, VVU na malaria, Bi. Moeti alionya.

“Athari, uwezekano, wa uamuzi huu itakuwa na uzito sana kwa kukomesha polio,” alisema Moeti, “wakati tu Afrika ilikuwa imekaribia kutangazwa bila polio.”

Trump alilaumu WHO yenye makao huko Geneva kwa kukuza “ukosefu wa taarifa” wa Kichina kuhusu virusi vya korona vipya, akisema hii ilikuwa pengine imefanya kuzuka kuwa kubaya zaidi na kwamba atakomesha ufadhili wake wa kifedha hata alivyotetea utunzaji wake wa tatizo.

Zaidi ya watu milioni 2 wameambukizwa ulimwenguni, na idadi kubwa zaidi nchini Marekani.

Washington ndio mfadhili mkubwa kwa WHO, ambayo hushughulikia magonjwa maalum na pia inaimarisha mifumo ya kiafya ya kitaifa. Marekani ilichanga zaidi ya dola milioni 400 kwa WHO mnamo mwaka wa 2019, takribani 15% ya bajeti yake.

“Tunatumai sana (kusimamishwa kwa ufadhili wa kifedha) kutafikiriwa tena kwa sababu serikali ya Marekani ni mshirika muhimu sio tu kwa masuala ya kifedha lakini kama mshirika muhimu wa kimkakati,” Moeti alisema.

Kuondolewa kwa kusitishwa kwa shughuli za kawaida kwa kiasi fulani nchini Ghana

“Kwa kuzingatia mafanikio madogo ya kudhibiti kuenea kwa virusi vya korona,” Rais Nana Akufo-Addo alitangaza kwa njia ya televisheni “kusitishwa kwa shughuli za kawaida kwa kiasi fulani huko Accra na Kumasi kumeondolewa.”

Miji minne mikubwa katika Accra Kuu, Ashanti na maeneo ya Katikati ilikuwa imesitishiwa shughuli za kawaida tangu Machi 31, kufuatia uthibitisho wa visa 137. Rais alisema uamuzi huo ulikuwa kwa msingi wa sayansi na data na hatua yoyote ya baadaye itaamuliwa na sababu hizi hizi. Alikubali, hata hivyo, athari mbaya ambayo usitishaji wa shughuli za kawaida ulisababishia maskini na wanyonge.

Hii inafanya Ghana kuwa nchi ya kwanza katika Afrika ya Sahara ndogo kuondoa vizuizi vya usafiri.

Kulingana na taarifa ya Bloomberg, idadi ya hivi karibuni zaidi ya maambukizi baada ya siku 21 za kizuizi cha usafiri ilikuwa 1,042.

Wakazi wa mji mkuu, Accra, na vituo vikubwa waliruhusiwa kurudi kazini ikianza ingawa vizuizi vingine kama vile kufungwa kwa shule na marufuku ya mikutano ya michezo na ya kidini inaendelea, Akufo-Addo alisema kwa njia ya televisheni.

Ugonjwa ulileta miaka mitatu ya upanuzi wa uchumi wa 6% au zaidi kukomeshwa ghafla katika taifa la watu milioni 30, na wizara ya fedha ikitabiri kwamba ukuaji unaweza kupungua hadi 1.5%, kiwango kidogo zaidi katika miaka 37.

Rais aliangazia mafanikio ya nchi, yaani kufanya kwa fujo ufuatiliaji wa mawasiliano ya watu walioambukizwa, kuimarisha uwezo wa kupima, kupanua idadi ya vituo vya matibabu na kutengwa, “kuelewa kwetu kuzuri kwa nguvu ya virusi, kuinua uwezo wetu wa majumbani kutengeneza vifaa vyetu vya kujikinga, sabuni na dawa.”

Marufuku juu ya mikusanyiko ya halaiki na kufungwa kwa mipaka ya Ghana kwa ulangusi wa binadamu, hata hivyo, vitaendelea kutekelezwa.

Tangazo hilo lilikua mshangao kwa wengine waliokuwa wakitarajia kupanuka au usitishaji wa shughuli za kawaida wa kitaifa kufuatia mwiba katika idadi ya visa vilivyothibitishwa nchini kote.

Hesabu ya kisa cha Ghana cha virusi vya korona imeongezeka maradufu tangu kisa cha kielezo kuripotiwa tarehe 12 Machi na imeenea hadi 10 za mikoa yake 16.

Kwa jumla ya visa 1,043, vingi viko Accra (882) na Kumasi (62). Kwa idadi hiyo, watu 99 wamepona na wameruhusiwa kwenda nyumbani ila tisa wamekufa.

Rwanda imetwikwa ‘mikopo’

Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani walinyoosha mikono yao mwezi huu kwa nchi zinazong’ang’ana barani Afrika, hivi karibuni waliidhinisha punguzo la deni la dola milioni 109.4 kwa Rwanda chini ya Mpango ulioimarishwa wa Nchi Masikini zenye Madeni Makubwa (HIPC).

Hii itatumika kukidhi mahitaji ya dharura ya salio la malipo ya Rwanda yanayotokana na kuzuka kwa janga la COVID-19, Hazina ilisema katika vyombo vya habari.

Athari ya kiuchumi ya janga la COVID-19 inajitokeza haraka, IMF iliendelea, huku mtazamo wa karibu ukidhoofika haraka. Hii imesababisha kuongezeka kwa mahitaji makubwa ya kifedha na fedha za nje. Mamlaka yamechukua hatua ya haraka kwa kuweka hatua za kusaidia kudhibiti na kupunguza kuenea kwa ugonjwa, walisema.

Fedha hizo zitatoa pesa kwa bajeti ya matumizi yaliyoongezeka yenye lengo la kudhibiti janga na kupunguza athari yake ya kiuchumi, ilibaini IMF. Lakini tofauti na ruzuku, fedha za IMF lazima zilipwe “kuhifadhi uendelevu wa deni katika kipindi cha kati.”

Wakopeshi wa kibinafsi wamekubali kwa hiari kusongesha au kutoa tena fedha dola bilioni 8 katika deni, chanzo cha wizara ya kifedha cha Ufaransa kilisema, lakini sio kulifuta, ikimaanisha kuwa faida itaendelea kuongezeka.

Hata Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alikubali kwamba nchi za Kiafrika zinapaswa kusaidiwa kwa “kufuta deni lao kabisa.”

David Himbara, profesa wa Rwanda-Canada, katika nakala iliyopewa jina: “(Rais) Kagame anaizamisha Rwanda katika Deni”, aligundua kuwa huu ni msururu wa pili na deni kubwa la nje kwa taifa la kati mwa Afrika. Chini ya Mpango wa IMF wa Nchi Maskini zenye Madeni Makubwa, baadhi ya dola bilioni 1.4 ziliondolewa katika wajibu wa Rwanda katika mwaka wa 2008, na kuacha dola milioni 668. Deni lake la jumla leo, kulingana na Saa ya Deni la Umma ni zaidi ya dola bilioni 13.

Kampeni ya Jubilee ya Deni yenye makao yake Uingereza inaongoza kushinikiza na vikundi karibu 140 vya kampeni na vya misaada kwa kufuta – sio kusitishwa – kwa malipo ya deni na nchi masikini zaidi.

Tim Jones, mkuu wa sera kwenye Kampeni ya Deni ya Jubilee, alisihi IMF na Benki ya Dunia kujisimamia malipo na kuwataka wawekezaji binafsi wasimamishe kuchukua malipo ya deni.

“Itakera ikiwa wawekezaji wa faida wa kibinafsi wataendelea kuchukua malipo ya faida kubwa kutoka kwa nchi masikini wakati huu wa shida,” Jones alisema. [IDN-InDepthNews – 22 Aprili 2020]

Kuenea kwa virusi vya korona kuliathiri Afrika na video iliyohuishwa na INPS-IDN.

NEWSLETTER

STRIVING

MAPTING

PARTNERS

Scroll to Top