Home – SDGs for All

A project of the Non-profit International Press Syndicate Group with IDN as the Flagship Agency in partnership with Soka Gakkai International in consultative status with ECOSOC

Watch out for our new project website https://sdgs-for-all.net

Angola ina Mpango wa Kuunda Vifaa vya Kijeshi vya Kirusi

share
tweet
pin it
share
share

Na Kester Kenn Klomegah*

MOSCOW (IDN) – Nchi nyingi za Afrika zinatafuta biashara yenye faida, uwekezaji na biashara badala ya misaada ya maendeleo. Sasa Angola, kusini ya kati ya Afrika, imetangaza mipango ya kampuni kupanua biashara yake ya kitaifa kutoka kwa kununua hadi kwa uundaji kamili wa vifaa vya kijeshi vya Kirusi kwa soko la kusini mwa Afrika, na ikiwezekana maeneo mengine katika Afrika – utambuzi unaokuja wa Kusudi la 16 la Maendeleo Endelevu unaotoa wito wa amani na haki.

Iwapo Angola inakuwa mtengenezaji mkuu na msambazaji wa silaha za Kirusi, daima kuna uwezekano baadhi ya silaha zinaweza hatimaye kuonekana nje ya Angola katika eneo la Ushirika wa Maendeleo wa Kusini mwa Afrika (SADC) wa wanachama 16, anaonya Profesa David Shinn katika Shule ya Elliott ya Masuala ya Kimataifa, Chuo Kikuu cha George Washington.

“Silaha zinazotengenezwa na nchi yoyote zinaweza na zinaonekana katika maeneo ya migogoro ya Kiafrika. Kuna nyaraka nyingi, kwa mfano, kwamba silaha zinazoundwa nchini China, Urusi na nchi za Magharibi zinatumika katika migogoro inayoendelea Darfur, mashariki mwa Kongo na Somalia,” anasema Profesa Shinn, Balozi wa zamani wa Marekani nchini Uhabeshi (1996-99) na Burkina Faso (1987-90).

Katika hali nyingine, serikali za Afrika zimehamisha silaha kwa vikundi vya waasi na silaha zingine nyingi zimenunuliwa kwenye soko la silaha la kimataifa, anaongeza.

Profesa Shinn aliongeza kuwa Afrika Kusini ina uwezo mkubwa zaidi wa kutengeneza vifaa vya kijeshi ikifuatiwa na Misri. Sudan, iliyopokea msaada kutoka China na Uajemi katika kujenga kiwanda chake cha silaha, na Nigeria, miongoni mwa zingine, pia ina uwezo wa kutengeneza vifaa vya kijeshi. Kwa maana hii, kile Angola inapendekeza kufanya (yaani, kuanzisha kiwanda cha kuunda) sio tofauti sana isipokuwa kwamba itasaidiwa na Shirikisho la Urusi.

Hata hivyo, Profesa Shinn ana matumaini kwamba mipango inayowezekana ya mauzo ya silaha za Angola itaidhinishwa na bunge la Angola, na kuwa ya manufaa kubwa kwa SADC, Umoja wa Afrika na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Mnamo Februari 29, 2019, Baraza la Usalama lilikubali azimio ambalo linaelezea hatua zinazoongoza kwa lengo la kukomesha mapigano barani Afrika kupitia ushirikiano wa kimataifa ulio bora na ushirika pamoja na usaidizi mkubwa wa shughuli za amani zinazoongozwa na Umoja wa Afrika.

Kwa sauti moja kukubali azimio la 2457 (2019) mwanzoni mwa mjadala wa ufunguzi wa siku ya muda mrefu, Baraza lilikaribisha uamuzi wa Umoja wa Afrika wa mataifa 54 kuondoa bara la mapigano kupitia njia yake ya “Kunyamazisha Bunduki barani Afrika ifikapo Mwaka wa 2020” mpango huo, kuonyesha utayari wake wa kuchangia lengo hilo.

Umuhimu wa azimio hili unasisitizwa na ukweli kwamba sasa kuna nchi kumi na tano za Afrika zinazohusika katika vita, au zinakabiliwa na mgogoro wa baada ya vita na mvutano. Katika Afrika Magharibi, nchi hizo ni pamoja na Côte d’Ivoire, Guinea, Liberia, Nigeria, Sierra Leone na Togo. Katika Afrika Mashariki, nchi hizo ni pamoja na Eritrea, Uhabeshi, Somalia, Sudan, Uganda.

Rais João Lourenço wa Angola alidhihirisha mpango wake wa kuunda silaha za Kirusi katika mahojiano ya kipekee kwa shirika la habari la Kirusi Itar-TASS wakati wa ziara yake rasmi ya siku nne ya Moscow kutoka Aprili 2-5, 2019. Alisema kuwa Angola ni mojawapo wa wanunuzi wakuu wa silaha za Kirusi na kwamba nchi yake inataka si tu kununua lakini pia kutengeneza.

“Kwa ushirikiano wetu wa kijeshi na kiufundi na Urusi, utaendelea na kuimarishwa. Tungependa kufuka kutoka kwa hali yetu ya sasa ya wanunuzi wa vifaa vya kijeshi vya Kirusi na teknolojia kuelekea kuwa waundaji na kuwa na kiwanda cha kutengeneza vifaa vya kijeshi vya Kirusi katika nchi yetu,” aliambia shirika la habari.

Ingawa hii ilikuwa ziara rasmi ya kwanza ya Lourenço nchini Urusi kama Rais wa Angola, ana ujuzi muhimu kuhusu mji mkuu wa Urusi, kwani alijifunza katika Chuo cha Kisiasa na Kijeshi kutoka 1978-1982.

Kwa miaka mingi, Urusi imefanya “ushirikiano wa kijeshi na kiufundi” sehemu muhimu ya malengo yake ya sera ya kigeni na Afrika. Kulingana na Waziri wa Ulinzi wa Angola Salviano de Jesus Sequeira, Urusi tayari imetoa ndege sita za kivita za SU-30K kwa Angola mwaka huu na zingine mbili zinatarajiwa ifikapo mwishoni mwa Mei.

Mbali na hilo, Sequeira alisema, nchi ina nia ya kununua mifumo ya ulinzi wa hewani ya Kirusi ya S-400, lakini hakuna mazungumzo kuhusu hili kwa sababu ya ugumu wa kiuchumi, na kuongeza kuwa “Jeshi la Angola hufanya kazi na silaha za Urusi.” Kwa sababu hiyo, ushirikiano wa kijeshi kati ya nchi hizo mbili utaendelea milele.

Kwa mujibu wa ripoti ya tovuti ya Wizara ya Ulinzi, Urusi ilikubali kusambaza silaha na vifaa vya kijeshi kwa Angola vyenye thamani ya dola bilioni 2.5 za Marekani, ikiwa ni pamoja na vyombo vya akiba vya silaha za Kirusi, silaha ndogo, risasi, mizinga, bunduki na helikopta zenye shughuli mbalimbali.

Katika ripoti ya utafiti iitwayo “Angola: Urusi na Angola – Kuzaliwa tena kwa Ushirika wa Kimkakati” uliotolewa na Chuo cha Masuala ya Kimataifa cha Afrika Kusini (SAIIA), waandishi Ana Christina Alves, Alexandra Arkhangelskaya na Vladimir Shubin walikubali kuwa “ulinzi unabaki kuwa mwelekeo wa ushirikiano imara wa Urusi na Angola. Hadi sasa, Urusi ni mshirika mkuu wa kijeshi wa kimkakati wa Angola.”

Ana Christina Alves, Mtafiti Mwandamizi katika Uwezo wa Kimataifa na Mpango wa Afrika wa SAIIA alieleza zaidi kuwa “vifaa vya kijeshi ni, bila shaka, upande mkubwa sana na wenye faida zaidi wa biashara ya Urusi na Afrika – ambayo takwimu kwa bahati mbaya hazina kipengele katika data rasmi ya biashara baina ya nchi. Kama haya yangejumuishwa, kipimo cha biashara baina ya nchi kingevutia sana. Hii ni, labda, mwelekeo wenye nguvu zaidi wa shughuli za kibiashara za Urusi barani Afrika kwa sasa, lakini kwa sababu ya hali ya biashara, machache sana yanajulikana nje ya duru za kijeshi, hivyo vigumu kupata picha halisi.”

Ushirikiano wa kijeshi na kiufundi kwa muda mrefu umekuwa kipaumbele katika mahusiano ya nchi mbili, na Umoja wa Soviet ulianza kusambaza silaha kwa vitengo vya waasi nyuma katika miaka ya 1960, Andrei Tokarev, Mkuu wa Kituo cha Mafunzo ya Kusini mwa Afrika katika Chuo cha Sayansi cha Urusi, aliiambia Kommersant, gazeti la kila siku la kifedha la Kirusi.

“Hata hivyo, kwa kuanguka kwa utawala wa ubaguzi wa rangi katika nchi jirani ya Afrika Kusini mwaka wa 1994 na mwisho wa vita vya wenyewe kwa wenyewe mwaka wa 2002, Angola haina maadui hasa, kwa hivyo haja ya vifaa vya silaha imepungua. Katika miaka ya hivi karibuni, uongozi wa Angola umekuwa na mipango ya kugeuza nchi kuwa msingi wa kukarabati vifaa vya Urusi kwa nchi za Afrika. kwa upande wake, Afrika Kusini ilikuwa na mawazo ya kibiashara kama hayo pia. Hakuna awezaye kupinga kwamba pendekezo kwa ununuzi wote na kutengeneza (kuunda) silaha ni jaribio la kuifanya Afrika Kusini ididimie, lakini kiwanda cha ndani hakijakuwa tayari kuunda vifaa vyake vya kijeshi,” alieleza Andrei Tokarev.

Wataalam wa kigeni pia walielezea wasiwasi wao. Profesa Alex Vines, Mkuu wa Mpango wa Afrika katika Chatham House, ambaye hivi karibuni aliwahi kuwa mwanachama wa Kikundi cha Wachunguzi wa Jumuiya ya Madola kwa Ghana katika mwaka wa 2016 na afisa wa uchaguzi wa Umoja wa Mataifa nchini Msumbiji na Angola, katika majadiliano ya barua pepe alikubali ushirikiano wa kijeshi na kiufundi wa Urusi na nchi za Kiafrika.

Aliandika barua pepe kutoka London kuwa “ushirikiano wa kijeshi wa Angola na Urusi umekuwa pamoja sana kwa miaka mingi na sehemu kubwa ya manunuzi kwa njia yake ya Simportex iko na Urusi. Hii inaendelea ambapo Urusi ilitoa ndege sita za kivita za aina ya SU-30K mwaka huu na [Angola] ina nia ya kufanya ununuzi wa mfumo wa ulinzi wa hewani wa S-400 wa Urusi. Maendeleo mapya yanatafuta ushirika na Urusi kwa ajili ya kuunda vifaa vya ulinzi nchini Angola. Urusi ina mfululizo wa vituo vya matengenezo barani Afrika . . . lakini haya yatakuwa maendeleo makubwa.”

Aidha, alisema kwamba uzoefu wake mwenyewe wa Angola, ikiwa ni pamoja na kuwa mkaguzi wa vikwazo wa Umoja wa Mataifa, “ni kwamba silaha za Angola hazijakuwa tatizo kubwa la wizi, lakini wasiwasi mkubwa ulikuwa uuzaji wa silaha za kale na risasi kutoka kwa stoo kuelekea madalali wa kujitegemea ambao baadaye waliuza vifaa kwa mashirika yaliyowekewa vikwazo.”

Profesa Shinn alisema katika mahojiano ya barua pepe kwamba hasa kwa mtazamo wa Angola baada ya kununuliwa kwa ndege aina ya SU-30K mtu anapaswa kuuliza kwa nini nchi inahitaji ndege yenye uwezo mkubwa wa kivita kama hiyo na adui ni nani hasa? [IDN-InDepthNews – 07 Aprili 2019]

NEWSLETTER

STRIVING

MAPTING

PARTNERS

Scroll to Top